Hebroni: Mafundisho
Habari Mpya
Loading...
Showing posts with label Mafundisho. Show all posts
Showing posts with label Mafundisho. Show all posts

Tuesday, May 10, 2016

ZIJUE BARAKA ZA KUJITOA

Wanafunzi wa kwanza wa Yesu wakaacha yote wakamfuata. Wengine waliacha nyavu zao, na wengine wakaacha shughuli zingine. Wengine waliacha familia zao kwa muda mrefu ili wahubiri injili. Wakristo wengi katika historia wamejitoa bila kuangalia faida zao wenyewe ili injili iwafikie watu wengine, na hivyo wamefanyika baraka kwa mataifa. Bila watu kujitoa ukristo ungekuwa umekufa zamani. Mtu anaweza kutoa mali, muda, kazi n.k. katika ufalme wa Mungu, lakini Biblia inatuonyesha kwamba hayo yote yanaanza kwa kujitoa mwenyewe, yaani moyo. Bila kujitoa mwenyewe hayo yote mengine hayana maana mbele za Mungu. (Mika 6:6-8)

Mtajiri na maskini anaweza kujitoa:

2 Kor 8:1-5 
Baadhi ya makanisa yalikuwa yameamua kuwasaidia wakristo wa Yerusalemu waliopatwa na shida ya njaa. Paulo anawaandikia Wakorintho akiwataja Wamakedonia kama mfano mzuri wa kujitoa. Wamakedonia walikuwa hawana mali nyingi. Wenyewe waliishi kwa shida. Hata hivyo walitoa hata kupita uwezo wao ili wasaidie wenzao huko Yerusalemu. Paulo anasema walijitoa nafsi zao kwanza kwa Bwana, na hata kwa ndugu zao katika imani.
2 Kor 8:7
Wakorintho ambao walikuwa hawakosi kitu waliambiwa watoe kwa ukarimu. Wajitoe wenyewe kama Wamakedonia walivofanya.

Yesu ni mfano mkuu wa kujitoa:

Rum 15:3 
2 Kor 8:9 
Fil 2:4-8 
Yn 3:16 
Kujitoa inamaanisha kujali mahitaji ya wengine. Usifikirie mahitji yako mwenyewe tu. Huenda mwenzako ana mahitaji makubwa kuliko wewe. Jirani yako huenda anapotea katika dhambi wakati wewe unatafuta mali ya dunia hii. Yesu alikuwa ana kila kitu alipoishi mbinguni, lakini akaamua kuzaliwa horini kama mtu maskini, na akafa msalabani ili sisi tusipotee.


Kwa nini tujitoe?

Fil 2:9-12
Kwa ajili ya kujitoa kwake Yesu Mungu akamwinua juu ya yote. Kwa nini Mungu akafanya hivyo?
Yn 12:24
Sheria ya kiroho inasema; Ili uhai upatikane, lazima kifo kiwepo kwanza. Unapojitoa kwa Mungu maisha yatakuwa yenye maana zaidi. Usipojitoa na moyo wako wote huenda utapotea, au utaokoka kwa neema, lakini utabaki kama mbegu pekee isiopandwa ardhini. Mbegu ikipandwa ardhini inazaa. Unapojitoa mia kwa mia unapandwa kama mbegu ardhini. Kwa namna fulani unakufa, lakini utazaa matunda. Mimi binafsi ninaomba nikifika mbele za Mungu siku moja nije pamoja na watu waliomwamini kwa sababu ya kujitoa kwangu.


Faida za kujitoa:

2 Kor 9:6-8

Faida ya kwanza: Mahitaji yako ya kila siku utayapata

Anayetoa mali, muda wake, nguvu zake na moyo wake wote kwa furaha na kwa hiari yake mwenyewe ameahidiwa kwamba mahitaji yake ya kila siku atayapata. Na Mungu anajaza kikombe chake mpaka kinafurika. Anapewa uwezo wa kutoa tena, na ngurudumu ya baraka kwake na kwa wengine inaanza kuzunguka.
2 Kor 9:13-14

Faida ya pili: Watu watakuombea.

Ukijitoa kwelikweli kwa Bwana utakuta watu wengine wanabarikiwa. Haitakuwa vigumu kwao kukukumbuka wanapomwomba Mungu. Mtu anayeombewa na wenzake anapata ushindi hata anapopita katika magumu maishani.

Faida ya tatu: Jina la Bwana litasifiwa.

Mkristo alieokoka ana lengo moja tu: kumtumikia Mungu. Mtu anapojitoa jina la Bwana linasifiwa. Ufalme wa Mungu unaenea. Mkristo wa kweli ataona hii ni faida kubwa sana.
Read more »

Sunday, May 8, 2016

Dalili za Mtumishi wa Mungu kwelikweli

– Mtumishi wa Mungu hawatawali washirika wa kanisa.
“Yesu akawaita, akawaambia, ‘Wafalme wa Mataifa huwatawala,…na wakubwa wao huwatumikisha. Lakini kwenu ninyi sivyo; bali mtu anayetaka kuwa mkubwa kwenu, atakuwa mtumishi wenu, na mtu anayetaka kuwa wa kwanza wenu, atakuwa mtumwa wa wote.” (Luka 22:25; Marko 10:42-44).
Mtumishi wa kweli hajifanyi kama ‘Bwana’ juu ya watu wa Mungu – hajiinui juu ya washirika kama ‘rais’ wa watu. Kumbuka, Bwana Yesu, Mwana wa Mungu, alisema ‘KWENU NINYI SIVYO’. Mchungaji huharibu sura ya Yesu machoni pa watu kama akitawala kama ‘mkuu wa kijiji’ juu ya washirika; ameacha tabia ya Yesu kama anajifanya ‘mkubwa’ kanisani. Hayo yote ni kosa kubwa sana. Kama mchungaji akiwatawala watu kwa nguvu, ndipo yeye hafuati Yesu. Paulo aliandika juu ya huduma yake, “Si kwamba tunatawala imani yenu; bali tu WASAIDIZI wa furaha yenu… Kwa maana hatujihubiri wenyewe, bali Kristo Yesu ya kuwa ni Bwana; na sisi wenyewe kuwa tu WATUMISHI WENU kwa ajili ya Yesu.” (2 Wakor.1:24; 4:5).
Mtume Petro aliwaandikia wazee/wachungaji ifuatyo: “lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia, si kwa kulazimishwa, bali kwa hiari kama Mungu atakavyo; si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo. WALA SI KAMA WAJIFANYAO MABWANA JUU YA MITAA YAO, bali kwa kujifanya VIELELEZO kwa lile kundi.” (Waebr.13:2,3). Inapaswa mtumishi wa Mungu awe kielelezo kwa washirika na siyo kujifanya ‘Bwana’. Bwana Yesu ametufundisha inapaswa awe ‘mtumishi’ au ‘mtumwa’ wa washirika!
– Kwa sababu ya upendo wake kwa kunid la Bwana, mtumishi wa Mungu yupo tayari kutoa maisha yake kwa ajili ya kundi la Bwana hata kama Yesu Kristo alivyofanya, “nasi tukiwatumaini KWA UPENDO MWINGI, tuliona furaha kuwapa, si Injili ya Mungu tu, BALI NA ROHO ZETU pia, kwa sababu mmekuwa wapendwa wetu.” (1 Wathes.2:8). Kwa hiyo…
– Mtumishi wa Mungu kwelikweli anawatumikia washirika kwa upole and unyenyekevu:
“bali tulikuwa wapole katikati yenu, kama vile mlezi awatunzavyo watoto wake mwenyewe… mimi Paulo mwenyewe nawasihi kwa upole na utaratibu wa Kristo; mimi niliye mnyenyekevu nikiwapo pamoja nanyi” (1 Wathes.2:7; 2 Wakor.10:1).
– Kwa maneno na matendo yake mtumishi wa kweli hachukizi dhamiri za washirika – dhamiri zao zinamshuhudia kwamba mwendo wake ni safi kabisa katika sehemu yote!
“tumekataa mambo ya aibu yaliyositirika, wala hatuenendi kwa hila, wala kulichanganya neno la Mungu na uongo; bali kwa kuidhihirisha iliyo kweli twajionyesha kuwa na haki, DHAMIRI ZA WATU ZIKITUSHUHUDIA MBELE ZA MUNGU…Ninyi ni mashahidi, na MUNGU PIA, jinsi tulivyokaa kwenu ninyi mnaoamini, kwa utakatifu, na kwa haki, bila kulaumiwa;  (2 Wakor.4:2; 1 Wathes.2:10). 
Hakuna sababu kumlaumu! “Tusiwe kwazo la namna yo yote katika jambo lo lote, ili utumishi wetu usilaumiwe.” (2 Wakor.6:3). Na hata Mungu ni shahidi mwendo wake! (1 Wathes.2:5).
– Mtumishi wa kweli wa Mungu HATAFUTI fedha zako. HATAMANI pesa zako wala hatakulazimisha umpe pesa kwa ajili ya huduma au maombi yake.
“Sikutamani fedha wala dhahabu, wala mavazi ya mtu.” (Matendo 20:33). Huyu ni mtumishi wa Mungu kwelikweli.
– Mtumishi wa Mungu HATAFUTI kujifanya mtajiri kupitia huduma yake kwako.
“Lakini Petro akasema, Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho.” (Mat.3:6). Mtume Petro pamoja na mitume wengine walipokea pesa nyingi sana kwa ajili ya waumini maskini lakini, kumbe, hawakuchukua pesa kwa ajili ya faida yao kujifanya matajiri! Hawakuishi kwenye nyumba ya fahari wala hawakuwa na walinzi wa binafsi. (Au unafakiri Petro au Paulo wangeweza kuwa na magari mengi ya gharama kubwa sana au kuishi katika nyumba ya fahari au kuwa na ndege ya binafsi kama ‘wahubiri’ wengine siku hizi? Je, unafikiri kuishi kwa fahari kama hiyo inawakilisha tabia ya Yesu Kristo?) Mitume wa Bwana walikuwa na moyo safi na walifanya huduma yao bila unyonyaji, “Maana hatukuwa na … maneno ya juujuu ya kuficha choyo; Mungu ni shahidi.” (1 Wathes.2:5). “Basi thawabu yangu ni nini? Ni hii, ya kuwa nihubiripo, nitaitoa Injili bila gharama, bila kutumia kwa utimilifu uwezo wangu nilio nao katika Injili.” (1 Wakor.9:18).
Neno la Mungu ni dhidi wachungaji ambao wanawahudumia watu Wake kwa ajili ya faida zao, kujitajirisha wenyewe. “Bwana MUNGU asema hivi; Ole wao wachungaji wa Israeli, wanaojilisha wenyewe; je! Haiwapasi wachungaji kuwalisha kondoo? …Mnawala walionona, mnajivika manyoya, …lakini hamwalishi kondoo.” Ezekieli 34:2,3.
– Mtumishi wa Mungu HATAFUTI vyake mwenyewe.
“Maana wote wanatafuta vyao wenyewe, sivyo vya Kristo Yesu.” Tutambue, Paulo anasema ‘wote’! Basi, kwa uhakika maana yake ni idadi isiyopungua ‘wengi’! Ina maana, watumishi wengi/wote (ila Timotheo) walitafuta vyao wenyewe! Walitumia huduma yao kwa ajili ya faida yao yenyewe. Jambo la kuhuzunishwa sana! Je, ni tofauti sana siku hizi?
– Mtumishi wa Mungu HATAFUTI kuwapendeza watu, hasemi mambo kwa kusudi la kuvuta watu kanisani kwake ili ajenge kanisa kubwa kwa ajili ya sifa yake.
“Kama ningekuwa hata sasa nawapendeza wanadamu, singekuwa mtumwa wa Kristo.” (Wagal.1:10). “Kama vile tulivyopata kibali kwa Mungu tuwekewe amana Injili, ndivyo tunenavyo; si kama wapendezao wanadamu, bali wampendezao Mungu. Maana hatukuwa na maneno ya kujipendekeza wakati wo wote, kama mjuavyo.” (1 Wathes.2:4,5).
– Mtumishi wa Mungu HATAFUTI sifa ya watu. “Hatukutafuta utukufu kwa wanadamu, wala kwenu, wala kwa wengine.” (1 Wathes.2:6). 
– Mtumishi wa Mungu HAVITAFUTI vitu vyako … wala faida yake! Anatafuta faida ya kiroho ya waumini.
“Maana sivitafuti vitu vyenu, bali nawatafuta ninyi…” 2 Wakor.12:14. Maneno ya ajabu! Mtume wa kweli anajitoa kwa ajili ya faida ya kiroho ya washirika!  Paulo alipenda waumini, siyo ‘vitu vyao’! Hatafuti vitu vyao, pesa zao, sifa zao au utukufu kwa watu! Mtumishi wa Mungu anajitoa kwa ajili ya faida ya wale awahudumiao. Anayo nia moja tu, “Maana nawaonea wivu, wivu wa Mungu; kwa kuwa naliwaposea mume mmoja, ili nimletee Kristo bikira safi.” (2 Wakor.11:2). Naye yupo tayari kujimwaga kwa ajili ya watu wa Mungu ili wapate faida ya kiroho, “Nami kwa furaha nyingi nitatapanya, tena nitatapanywa kwa ajili ya roho zenu. Hata kama kadiri nizidivyo kuwapenda sana, ninapungukiwa kupendwa.” (2 Wakor.12:15).
Maneno ya kuchanga moto! Mtumishi ya Mungu huzidi kuwapenda waumini awahudumiao hata hivyo anapungukiwa kupendwa!
– Mtumishi anamtegemea Mungu kwa ajili ya mahitaji yake.
“Si kwamba nasema haya kwa kuwa nina mahitaji; MAANA NIMEJIFUNZA KUWA RADHI NA HALI YO YOTE NILIYO NAYO. Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; KATIKA HALI YO YOTE, na katika mambo yo yote, nimefundishwa KUSHIBA NA KUONA NJAA, kuwa na vingi na kupungukiwa. Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.” (Wafilipi 4:11-13).
– Mtumishi wa Mungu hufurahi kwa ajili ya waumini wanapotambua ni jambo la haki na la pendo kumsaidia mtumishi ambaye anafanya kazi mbele ya Mungu kwa ajili yao.
“Nalifurahi sana katika Bwana, kwa kuwa sasa mwisho mmehuisha tena fikira zenu kwa ajili yangu, kama vile mlivyokuwa mkinifikiri hali yangu lakini hamkupata nafasi….Lakini mlifanya vema, mliposhiriki nami katika dhiki yangu…. hakuna kanisa lingine lililoshirikiana nami katika habari hii ya kutoa na kupokea, ila ninyi peke yenu. Kwa kuwa hata huko Thesalonike mliniletea msaada kwa mahitaji yangu, wala si mara moja. SI KWAMBA NAKITAMANI KILE KIPAWA, bali nayatamani mazao yanayozidi kuwa mengi, KATIKA HESABU YENU. Lakini ninavyo vitu vyote na kuzidi, tena nimejaa tele; nimepokea kwa mkono wa Epafrodito vitu vile vilivyotoka kwenu, HARUFU YA MANUKATO, sadaka yenye kibali, IMPENDEZAYO MUNGU.”
Ndiyo. Paulo alikuwa na mahitaji na alipokea kile kipawa kwa ajili ya MAHITAJI yake (SIYO KWA AJILI KUMFANYA MTAJIRI) kwa furaha – lakini siyo kutokana na uchoyo au tamani yake apate fedha, lakini alifurahi KWA AJILI YA WAUMINI TU. Katika utoaji wao Paulo alitambua matunda ya pendo katika maisha yao ambayo ni kama harufu ya manukato impendezayo Mungu! Alifurahi kwa ajili ya hayo tu! Tena ni wazi hapo kwamba mtumishi wa Mungu hawalazimishi waumini wamtoe pesa. Anafurahi waumini watoe kipawa kwa hiari kutokana na pendo la Mungu mioyoni mwao!
Ni kweli kabisa, na neno la Mungu linatufundisha kwamba ni jambo la haki na la pendo kuwasaidia watumishi wa Mungu SAWASAWA NA MAHITAJI YAO kama wanajitoa kwa ajili yetu. Lakini ndani ya moyo wa mtumishi wa Mungu kwelikweli hamna uchoyo au tamani kwa pesa, kwa sifa, kwa kujiinua, kwa kujifanya mtajiri au kuishi kwa fahari, wala hawalizimishi watu wa Mungu kumpa pesa.
© 2016  David Stamen    somabiblia.com
Read more »

Saturday, May 7, 2016

FAHAMU VYAKULA UNAVYOTAKIWA KULA ILI KUJENGA AFYA YAKO PASIPO GHALAMA KUBWA

Katika sehemu nyingi duniani, watu wengi zaidi hula chakula kikuu chenye bei nafuu ndani ya kila mlo. Chakula hicho kikuu huwapatia nguvu ya kutosha kuwawezesha kutimiza mahitaji yao ya kila siku. Lakini chakula hicho kikuu pekee hakitoshi kumfanya mtu awe mwenye afya. Kuweza kukua, kuwa na nguvu, na kupambana na maambukizi, lazima tule vyakula vingine-zaidi ya chakula kikuu.
Uji ambao haujachanganywa na chochote hautoshi.
Ongezea maharagwe, nyama, maziwa, mayai, mbogamboga,au matunda.


Kwa ajili ya afya bora, tunahitaji:.....BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Read more »

Sunday, May 1, 2016

ROHO YA HEKIMA NA UFUNUO KATIKA KUMJUA YEYE

1
Na: Patrick Sanga

Salaam katika jina lake BWANA Yesu
Katika Waefeso 1:17 Biblia inasema ‘Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu, awape ninyi ROHO YA HEKIMA NA YA UFUNUO KATIKA KUMJUA YEYE’. Hili moja ya maombi muhimu ambayo Mtume Paulo alifanya kwa jili ya Kanisa la Efeso. Kila nisomapo mstari huu nimekuwa nikijuliza sana ni kwa nini Mtume Paulo aliomba maombi haya kwa kanisa hili?.
Katika kutafakari na kuendelea kujifunza niligundua kwamba kulikuwa na sababu kubwa tatu ambazo zilimpelekea Mtume Paulo kuwaombea jambo hili, na kutokana na umuhimu wake hata kwa kanisa la sasa ndiyo maana nimeona ni vema nikaliandika hapa ili na wewe msomaji uweze kujifunza.
Zifuatazo ni sababu kadhaa zilizompelekea Mtume Paulo aliombee kanisa la Efeso roho ya hekima na ufunuo na kwa sababu hiyo zinatusaidia kujua umuhimu wake kwa kanisa la sasa pia;
Ili waweze kumjua Mungu zaidi (Waefeso 1:17)
Waefeso 1:11 ‘Na ndani yake sisi nasi tulifanywa urithi, huku tukichaguliwa tangu awali sawasawa na kusudi lake yeye, ambaye hufanya mambo yote kwa shauri la mapenzi yake’.
4
Kazi ya roho ya ufunuo ni kumfunua Mungu kwa kiwango ambacho bado hujakiona wala kukizoea ili kuboresha uhusiano wako na Mungu na kukufanya umaanishe katika kumpenda. Ndiyo, lengo ni kumfunua Mungu kwako, kutoka kwenye kona tofauti tofauti ili umjue zaidi ili hali kazi ya roho ya hekima ni kukupa ufahamu (maarifa), werevu na busara katika kufanya maamuzi sahihi kuhusu uhusiano wako na Mungu na maisha yako kwa ujumla. Katika ufunuo kuna mambo ambayo Mungu atayaleta kwako na yanahitaji hekima katika kuyafasiri, kuyanena na kutenda.
Naam bado hatumjui Mungu kwa kiwango kitupasacho kumjua na ndio maana tunahitaji roho ya ufunuo. Roho ya ufunuo inamuongoza mtu kujenga mahusaino binafsi na Mungu wake tokana na ufunuo aliopata.  Roho hii inatuleta kwenye ufahamu muhimu kuhusu ulimwengu wa roho na kwamba ni lazima tuanze kuishi maisha katika ulimwengu wa roho kuliko vile tunavyoishi katika ulimwengu wa mwili ili kumjua Mungu zaidi.
Ili kujua mambo ambayo Mungu amewaandalia (1Wakorinto 2:9-10)
Katika fungu hilo Biblia inasema hivi ‘Lakini, kama ilivyoandikwa, MAMBO AMBAYO JICHO HALIKUYAONA WALA SIKIO HALIKUYASIKIA, (Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,) Mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao. LAKINI MUNGU AMETUFUNULIA SISI KWA ROHO. Maana Roho huchunguza yote, hata MAFUMBO ya Mungu’. Pia katika Waefeso 1:18 imeandikwa ‘MACHO YA MIOYO YENU YATIWE NURU MJUE tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo’
5
Mungu anataka watu wake wajue kwamba yeye anayo mawazo (Yeremia 29:11), mbalimbali ambayo amewaandalia watoto wake. Mawazo hayo yameunganishwa na kusudi la kuwepo kwao hapa duniani na hawana budi kuyajua, kuyapata na kuyatenda. Naam ili wafikie hapo sharti juu yao na ndani yao, wawe na roho ya hekima na ufunuo.
Kumbuka katika kila nyanja ya maisha iwe kazi, uchumi, biashara, familia, huduma, ndoa nk, yapo mambo ambayo ameyaandaa na anataka uyajue. Naam ni jukumu lako kuendelea kujenga na kuboresha mahusaino yako na Roho Mtakatifu yawe mazuri daima.
Ili kuujenga mwili wa Kristo ipasavyo
Katika 1Wakorinto 12:7 Biblia inasema ‘Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana’.  Ukiendelea Katika 1Wakorinto 12:20 imeandikwa ‘Na jicho haliwezi kuuambia mkono, sina haja na wewe; wala tena kichwa hakiwezi kuaimbia miguu; sina haja na ninyi’ na ule mstari wa 25 unasema ‘Ili kusiwe na faraka katika mwili, BALI VIUNGO VITUNZANE KILA KIUNGO NA MWENZIWE(1Wakorinto 12:25).
Hivyo roho ya ufunuo inatoa ufunuo ili kufaidiana, lengo ikiwa ni kuusaidia mwili wa Kristo kuimarika zaidi. Naam kumbuka ufunuo huu ni kwa sehemu kwa lengo la kulijenga kanisa, mwili wa Kristo. Katika 1Wakorinto 12:11 imeandikwa ‘Lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye’. Na tena Mtume Paulo anamalizia kwa kusema ‘Basi ninyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake’ (1Wakorinto 12:27).
Naam hakuna mtu anayepewa karama zote, kila mmoja anapewa kwa SEHEMU kama KIUNGO ili kwa kushirikiana, MWILI wa Kristo ujengwe vema. Naam kila kiuingo lazima kihakikishe kina kuwa na ufanisi unaotakiwa, si kwa ajii yake, bali kuhakikisha mwili wa Kristo unajengwa ipasavyo, kupitia ufunuo/uwepo wa kile kiungo.
Kanisa lazima lifike mahali pa kuwa na uelewa kamili juu ya mwili wa Kristo unavyopaswa kutenda kazi kupitia ufunuo wa Roho Mtakatifu kwa kuwa ‘Mungu amevitia viungo kila kimoja katika mwili kama alivyotaka (1Wakorinto 12:18). Naam kila mshirika unayemuona NI KIUNGO CHA MWILI WA KRISTO KUPITA KARAMA, VIPAWA NA HUDUMA ALIZOPEWA kwa lengo la kuujenga mwili wa Kristo.  Roho ya hekima ikuongoze kutenda na kujua kwamba karama, huduma na vipawa ulivyonavyo ni kwa ajili ya kuujenga mwili wa kristo.
Naam hatupaswi kumdharau mtu yoyote kutokana na hali yake ya nje kwa jinsi ya kibinadamu maana yeye ni kiungo kinachostahili heshima zaidi (1 Wakorinto 12:22) Kazi ya Mchungaji na viongozi wa kanisa ni kufuatilia ili kujua Mungu ameweka/ametoa/amefunua kitu gani (karama/vipawa/huduma) juu ya wale wanaowaongoza ili kuviendeleza kwa lengo la kuujenga mwili wa Kristo.
3
Hivyo tokana na umuhimu wa roho ya hekima na ufunuo juu ya kanisa la Mungu na kwa mtu mmoja mmoja ni vizuri tukachukua au ukachukua hatua ya kuanza kumomba Mungu akujalie roho ya hekima na ufunuo wewe binafsi, familia yako, jamaa zako na kanisa kwa ujumla ili manufaa yake yawe dhahiri katika mwili wa Kristo ulimwenguni kote.
Roho ya hekima na ufunuo na iwe nanyi
Utukufu na heshima vina wewe Yesu, wastahili BWANA!
cHANZO: Sanga
Read more »

Tuesday, February 2, 2016

UJUMBE wa Neno la MUNGU


5 Katika shida yangu nalimwita Bwana; Bwana akanijibu akaniweka panapo nafasi.
 6 Bwana yuko upande wangu, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?
 7 Bwana yuko upande wangu, msaidizi wangu, Kwa hiyo nitawaona wanaonichukia wameshindwa.
 8 Ni heri kumkimbilia Bwana Kuliko kuwatumainia wanadamu.
 9 Ni heri kumkimbilia Bwana. Kuliko kuwatumainia wakuu.
 10 Mataifa yote walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
 11 Walinizunguka, naam, walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
 12 Walinizunguka kama nyuki, Walizimika kama moto wa miibani; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
 13 Ulinisukuma sana ili nianguke; Lakini Bwana akanisaidia.
 14 Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu, Naye amekuwa wokovu wangu.
 15 Sauti ya furaha na wokovu Imo hemani mwao wenye haki; Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu.
 16 Mkono wa kuume wa Bwana umetukuzwa; Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu.
 17 Sitakufa bali nitaishi, Nami nitayasimulia matendo ya Bwana
(Zab 118:5-17)
UBARIKIWE NA NENO
Read more »

Wednesday, January 27, 2016

Siri ya Maombi/Ombi Linalojibiwa

Anatoli Levitini, mwandishi na mwanahistoria wa Kirusi, alitumia miaka yake mingi katika Gulag ya Siberia, ambako dua zilizotolewa kwa Mungu zilionekana kana kwamba zimeganda ardhini. Lakini alirudi akiwa mzima kiroho. "Mwujiza mkuu kuliko yote ni maombi," aliandika. "Yanipasa tu kumgeukia Mungu kimawazo na mara moja naisikia nguvu inayoingia ndani yangu kutoka mahali fulani, inaingia katika roho yangu, na mwili wangu wote. Je! hicho ni kitu gani? Je, naweza kuipata wapi hiyo nguvu inifanyayo mimi kuwa mtu mpya na kuniokoa mimi, niliye mzee duni sana, niliyechoka na maisha, ambayo itaniinua juu ya dunia hii? Inatoka nje yangu - wala hakuna nguvu yo yote ulimwenguni humu ambyo ingeweza kuipinga."
Katika mwongozo huu tunaona jinsi maombi yanavyotusaidia kujenga uhusiano wenye nguvu zaidi pamoja na maisha ya Kikristo yenye nguvu.
1. Kuzungumza Na Mungu
Je, tunawezaje kuwa na uhakika kwamba Mungu anatusikia tunapoomba?
"Ndipo mtaniita mimi na kwenda KUNIOMBA, nami NITA SIKILIZA. Nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote." - Yeremia 29:12,13.
Je, ni uthibitisho gani aliotoa Yesu kuonyesha kwamba atasikia na kujibu maombi yetu?
"Basi nawaambia, Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, na mlango utafunguliwa kwenu." - Luka 11:9.
Maombi ni maongezi ya pande mbili. Hii ndiyo maana Yesu anaahidi anasema:
"Tazama nasimama mlangoni, nabisha. Mtu ye yote akiisikia sauti yangu, na kuufungua malngo, nitaingia na kula pamoja naye, na yeye pamoja nami." - Ufunuo 3:20.
Kwa jinsi gani inawezekana kwetu kuketi na kuwa na maongezi mazuri wakati wa chakula cha jioni pamoja na Kristo? Kwanza, kwa kumwambia kila kitu tulicho nacho moyoni mwetu kwa njia ya maombi. Pili, kwa kusikiliza kwa makini. Tunapotafakari wakati wa maombi, Mungu anaweza kuongea nasi moja kwa moja. Na tunapolisoma Neno la Mungu kwa roho ya ibada, Mungu ataweza kuongea nasi kupitia katika kurasa zake.
Maombi yanaweza kuwa njia ya maisha kwa Mkristo.
"OMBENI BILA KUKOMA; shukuruni kwa kila jambo, maana hayo ndiyo mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu." - 1 Wathesalonike 5:16-18.
Je! sisi tunawezaje "kuomba bila kukoma?" Je, yatupasa kupiga magoti wakati wote au kurudia-rudia kusema maneno ya kumsifu au kutoa dua? La, hasha. Lakini tunapaswa kuishi karibu sana na Yesu kiasi cha kujisikia huru kusema naye wakati wo wote, na mahali po pote.
"Tukiwa katika makundi ya watu mitaani, katika shughuli ya kibiashara, tunaweza kutoa dua yetu kwa Mungu na kumsihi atupe uongozi wake… Daima tungeacha wazi mlango wa moyo wetu na kuuacha mwaliko wetu ukipanda juu ili Yesu aweze kuja moyoni mwetu na kukaa humo kama mgeni wetu wa mbinguni." - Steps to Christ, uk. 99.
Read more »

Monday, January 18, 2016

KIJANA USITAFUTE KICHAKA, JISALIMISHE KWA YESU

Bwana Yesu asifiwe!. Mtumishi wa Mungu Godfrey Miyonjo kupitia ujumbe huu ambao Mungu amempa anazungumza na wewe kijana unayetafuta kichaka cha kujificha ili uendelee na dhambi zako ili sasa uokoke na utoke huko kichakani. Dawa ya dhambi ni kumpa Yesu maisha yako. Endelea sasa kusoma ujumbe huu na Mungu akubariki sana (Mwl. Daudi, JL. VIJANA NA UTUMISHI).
“Kisha wakasikia sauti ya BWANA Mungu, akitembea bustanini wakati wa jua kupunga; Adamu na mkewe wakajificha kati ya miti ya bustani, BWANA Mungu asiwaone”
MWANZO 3:8.
BWANA YESU asifiwe.
Wapendwa ninawasalimu kupitia jina La Yesu,
Binafsi Ninamshukuru Mungu anayenitetea hadi hivi leo.
Ni Mungu pekee ndiye atupiganiaye na kutuepusha na mabaya yote ambayo yule mwovu hukusudia juu yetu.
Mtu wa Mungu, BWANA amesema nami ili niseme na wewe kuwa “USITAFUTE KICHAKA”
Kwa maana sisi wanadamu hatuna uwezo wa kujificha mbele za Mungu ili asituone.
Ijapokuwa akili zetu zinatudanganya kuwa twaweza kujificha mbele za Mungu ili asituone, lakini ukweli ni kwamba hatuna uwezo huo.

Read more »

Sunday, January 17, 2016

Dr. Myles Monroe on Understanding Kingdom Principles


Listen to the speech below


Read more »

ANGALIA NAMNA MASHAKA NA UOGA JINSI VINAVYOKWAMISHA MAHALI UNAPOPASWA KUFIKA....

woga

Usipoweza kujikana na kuthubutu, hutoweza kamilisha mambo makubwa” C,S Lewis

Watu wengi wamekuwa wanatamani sana kuwa na maisha yaliyo bora na kuwa na hali njema kiroho lakini miongoni mwa vikwazo vya kuwa hivyo licha ya kile cha watu wa karibu yao/marafiki, changamoto nyingine ni uoga/mashaka.  

Uoga ni ile hali ya kusitasita kuthubutu kufanya mambo na kuweka mashaka kama matokeo yatarajiwayo yanaweza kutokea. Mara zote hali hii uambatana na maneno kama;

Sidhani.

Siwezi

Sijui.

Labda.

Nitajaribu badala ya nitafanya.

Kibiblia hii ni hali ya kukosa uhakika na ubayana juu ya mambo yatarajiwayo na mambo yasiyoonekana; yaani ni kukosa imani. Na kitendo hiki kinamfanya mtu wa Mungu kuishi maisha yanayomfanya Mungu asiwe na furaha kwa kuwa haiwezekani kumpendeza Mungu pasipo kuwa na imani.

Waebrania 10:38-39 “Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye. 39 Lakini sisi hatumo miongoni mwao wasitao na kupotea, bali tumo miongoni mwa hao walio na imani ya kutuokoa roho zetu.”

Waebrania 10:6a “Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza;……..”

                Uoga ni kitendo cha kupungukiwa imani kwa kuingiwa na wasiwasi.

Marko 4:40 “Akawaambia, Mbona mmekuwa waoga? Hamna imani bado?”

Yesu anaweka uwiano wa maneno mawili ya ‘kuwa waoga’ na ‘kukosa imani’ Kwa kumaanisha kuwa wanafunzi waliogopa kwa kuwa hawakuwa na imani bado na kama wasingekuwa waoga ni matokeo ya kuwa na imani na kama wangekuwa hivyo Yesu angeweza kunena nao na kusema “hamkuwa waoga, mmekuwa na imani sasa”.

Read more »

How To Overcome Bad Habits

63633ea3fd765bf24e462481e43a6113
On Fridays, I post excerpts from the writings of the great American bishop and media evangelist, Ven. Fulton J. Sheen. I call them #FultonFridays.
“I have a bad temper,” or “I drink too much”—“”I am always criticizing,” or “I am lazy” are familiar complaints from those who still believe that nobility of character is an important goal. They would not make such admissions if they did not have a strong desire to break the chain of evil habits. They can realize this desire—any bad habit can be broken. But getting free of it requires four things:
Introspection is necessary in order that we shall isolate the habit and see it clearly as a sin. The surprise we feel when others criticize some fault in us proves that we have not practiced introspection sufficiently to know ourselves. Some people are afraid ever to look into their consciences, for frear of what they might find; they are like the other cowards who dare not open telegrams because they dread bad news.
Read more »

Thursday, January 14, 2016

SOMO: Uchumba ni nini? na Ndoa ni nini?


Shalom, wapendwa,
Katika somo letu leo nataka tuangalie vitu hivi viwili, mahusiano ya uchumba na mahusiano ya ndoa. Sifa za mahusiano ya uchumba na sifa za mahusiano ya ndoa. Kwa nini nataka tujifunze somo hili? Kwa sababu siku hizi za leo kumekuwa hakuna tofauti kati ya uchumba na ndoa, hali hii imeingia mpaka makanisani.
Inashangaza sana, leo wachumba wanafunga ndoa tayari wakiwa wameishakuwa wanandoa, tena wengine wanasubiri wapate watoto wakiwa bado wachumba eti ndio wafunge ndoa. Lakini mbali na hayo, bado namna wachumba wanavyoendesha mahusiano yao yanatafsiri mahusiano ya ndoa, japokuwa ukiwauliza wanasema wao ni wachumba.

Uchumba ni nini, mipaka yake na miiko yake ni ipi? 
Uchumba ni mahusiano ya awali ambayo wawili (mwanamume na mwanamke) ambao bado hawajaingia ktk ndoa wanakubaliana kuoana, na hivyo wanaanzisha mahusiono ya karibu. Makubaliano yao hayo yanaonyesha; 1. Nia yao ya dhati kuwa wanandoa hapo baadae, 2. Maamuzi ya dhati ambayo kila mmoja ameamua kuchukua, na 3. Kwamba kila mmoja amemkubali mwenzake na kwa sababu hiyo anajiandaa kuwa mwenzi wa ndoa wa mwenzake wakati mfupi ujao. Kwa sababu hiyo. Kwa maana nyingine mahusiano ya uchumba ni maandalizi ya pamoja ya mwisho kabla ya ndoa baada ya hawa wawili kujiandaa kila mmoja kwa nafasi na wakati wake. Sasa hapa baada ya kuridhiana kuwa wataoana wanaanza kufanya maandalizi ya pamoja ya mwisho mapema kabla ya ndoa. Kwa hiyo maandalizi ya kuingia ktk ndoa si ndoa. 

Kwa sababu hiyo mtaishi kama kaka na dada kwa kipindi chote cha mahusiano yenu ya uchumba. 

Alama kubwa katika mwenendo wa mahusiano haya ni HESHIMA YA KAKA NA DADA, wakati wote wa mahusiano ya uchumba na si zaidi ya hapo. Zaidi ya hapo, wahusika watajaribiwa kuwa wanandoa wakati wa uchumba wao. Ikumbukwe, uchumba si ndoa, ni mlango utakaowawezesha wawili hawa kwa pamoja wakiwa wamepatana na kukubaliana huku wakiwa kila mmoja amemridhia mwenzake kuingia ktk ndoa kwa agano. Kwa hiyo, uchumba haukuhalalishii kuwa uliyenaye kwenye mahusiano hayo wakati huo ni mume au mke wako. Hivyo, basi, mtakachokuwa mkifanya kwa kipindi chote cha uchumba ni maandalizi ya kuingia ktk ndoa huku kila mmoja akimuheshimu mwenzake kama dada yake au kama kaka yake. Mtatumia Muda huu kupanga mipango ya maisha yenu, kufahamiana kihulka na kitabia, kikubwa zaidi ni kuweka msingi wa ndoa yenu. Kumbuka, hamuwezi kuishi zaidi ya maandalizi mliyoyafanya. Kama hamtajipanga wakati wa uchumba, mkafanya makubaliano ya pamoja ktk baadhi ya mambo au mambo yote yanayowahusu mtashindwana na mtapishana kwa kila jambo wakati wa ndoa. 

Pia, pamoja na kuwa uchumba si ndoa lkn pia sio uwanja wa utakaotumia kuntafuta anayekufaa. Mahusiano haya ni kwa ajili ya wale tu wenye uhakika, waliothibitisha kuwa nitamuoa huyu au nitaolewa na huyu. Na kwa sababu hiyo kama huna uhakika usichumbie, na wala usikubali kuchumbiwa. Kwa nn umuambie mwanamke kuwa unampenda wakati unajua kabisa au huna uhakika kwamba utamuoa.

Au kwa nini umkubalie mwanaume aliyekuambia anakupenda na anataka kukuoa wakati una uhakika kwamba huwezi kuolewa naye au hauna uhakika wa kuolewa naye.

Unapochumbia na unapochumbiwa na ukakubali kusudia kutokuachana, isije baadae ukasema haukuwa mpango wa Mungu, sasa uliingiaje? Bila shaka hukujiandaa. Lkn kumbuka kukosa kwako maandalizi kutasababisha maumivu kwa mwenzako. 

Mtu huingia kwenye mahusiano ya uchumba baada ya kuwa ameishafanya maamuzi, ana uhakika na maamuzi yake, na yuko tayari kuyasimamia kwa gharama yoyote. Usikubali kuachana. Mkisha kubaliana, kuachana Mungu hapendi, anachukia. Kama Mungu hapendi kuachana, basi kila unapoachana na mwenzi wako anachukia. Jiulize, Mungu amechukia mara ngapi kwa upande wako, umeachana mara ngapi na wewe ukiwa ndio sababu? 

Tuangalie Kuhusu Ndoa japo kwa sehemu tu. 
Ndoa ni agano lenye kusudi la wawili (Mwanamume na mwanamke) kuishi pamoja kama mwili mmoja maisha yao yote baada ya kukubaliana, kila mmoja akimkubali mwenzake kuishi na kuwa naye wakati wote ktk hali zote kwa moyo wake wote.
Katika ngazi hii ya mahusiano ndipo watu huwa mke na mume kwa kuunganishwa na Mungu kuwa mwili mmoja. Na ktk ngazi hii tendo la ndoa uhusika, na mambo yote ya faragha yahusuyo upendo, na si ktk uchumba. Huwezi kuishi maisha ya ndoa wakati wa uchumba; ukashiriki tendo la ndoa, na kufanya mambo ya faragha ya upendo na yale yasiyo ya faragha lkn yanawahusu zaidi wana ndoa. Kufanya hivyo ni kuharibu ndoa yenu, lkn kuhatarisha mahusiono yako ya uchumba. 

Unaposhiriki mambo ya ndoa wakati wa uchumba unajijengea na unamjengea mwenzi wako tabia ya kukosa uaminifu ktk ndoa yenu na hivyo kuwa wachepukaji wakati wa ndoa. Lakini pia kufanya hivyo ni kumpa ibilisi nafasi ktk uchumba wenu, na lazima ataharibu tu, asipoharibu kwenye uchumba ataharibu kwenye ndoa, hawezi kuwaacha ivi hivi ikiwa mmempa nafasi. Na kati ya watu wanatumia nafasi bila kupoteza iwapo wataipata, ni shetani. Kwa hiyo kuwa mwangalifu sana. 
Usipoteze uzaliwa wako wa kwanza na mbaraka wako kwa kipande cha mkate ambacho utamu wake haudumu kinywani na ujazo wake haujazi tumbo milele. Japokuwa ni kitamu kitatupwa chooni na wala hutabaki chooni ukifurahi kukitazama. Jitunze, mtunze mwenzi wako, tunza uchumba wako, tunza ndoa yako. Matunzo yanaanza kwa wewe kujitunza, kumtunza mwenzi wako, kutunza uchumba wako na hatimaye kutunza ndoa yako. 

Ubarikiwe na Bwana, 
Wako, Mch. Ezekiel P. Bundala

Crdit>Kanisa Forum
Read more »
 

Followers


LinkWithin

Hebroni 2016. Powered by Blogger.